
Kila mtu ana story yake kwenye maisha na haijalishi ni wakati mgumu kiasi gani unapitia kwenye maisha yako tambua kila mtu anapitia magumu yake. Lucas Malembo ni mwanzilishi wa "Malembo Farm" inayojishughulisha na maswala yote ya kilimo, Malembo ana amini kua kilimo kinaweza kutengeneza ajira kwa vijana wengi na vile vile kuikuza nchi yetu ki uchumi. Wengi tumemzoea Lucas Malembo akiongelea kilimo mara kwa mara ila kwenye episode hii amegusia mambo aliyopitia kwenye maisha yake kupelekea kuzaliwa kwa "Malembo Farm". Ni matumaini yangu utafurahia mahojiano haya na kujifunza mambo mengi
Oct 21, 2022
1 hr 24 min

Kwenye maisha ya kila siku watu napitia mambo mengi ikiwemo kutafuta hela, stress za familia, stress za kazi n.k na mitandao inabidi iwe sehemu ya mtu kupata furaha hata kama siku yake ilikua mbaya kiasi gani. Kupitia mtandao wa twitter kuna kijana anaitwa "Big0047" yeye huwa anatengeneza memes kwa njia ya picha na watu wengi wamekua wakifurahishwa na ubunifu wake. Tumeongea kuhusu mtandao uliompa yeye umaarafu na story nyingine kibao kumuhusu yeye. Natumaini utaenjoy mahojiano haya.
Oct 14, 2022
58 min

Mwalimu ni mtu muhimu sana kwenye maisha yetu na walimu wamebadilisha maisha ya watu wengi sana. Leo nimefanya mahojiano na mwalimu wa watoto wadogo ambae amejichukulia umaarufu mkubwa sana kwenye mitandao ya kijamii, tumezungumzia mambo mengi ikiwemo pia safari yake ya maisha mpaka kufikia hapo alipofikia sasa ivi na jinsi gani kumpoteza mama ake kulimfanya apitie kipindi kigumu sana kwenye maisha yake. Ni matumaini yangu utafurahia mahojiano haya na pia kuna kitu utajifunza.
May 21, 2021
57 min

Episode hii nimeifanya special kwa ajili ya valentine kilichonifanya niwachague Mr & Mrs Mrusi ni kwa sababu wapenzi hawa twitter ndo iliwakutanisha kwa mara ya kwanza na baada ya hapo kufikia maamuzi ya kuoana, kwenye Episode hii tumezungumza mambo mengi kuhusu mahusiano na ndoa vile vile tumegusia maisha ya wawili hawa ndani ya ndoa. #PHONECALLBYFOTTY
Feb 15, 2021
48 min
Load more






